Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 3, 2014

'Serikali ya Kenya haitaki mazungumzo na upinzani'

Muungano wa Jubilee unaoongoza serikali ya Kenya umeketaa takwa la muungano wa upinzani ujulikanao kama Cord la kutaka mazungumzo ya kitaifa yafanyike siku ya Julai Saba maarufu kama Saba Saba.
Akizungumza baada ya mkutano wa wabunge na maseneta wa Jubilee katika Ikulu ya Rais mjini Nairobi, Kiongozi wa Waliowengi katika Bunge la Taifa la Kenya, Aden Duale, amesema, mazungumzo yoyote ya kitaifa yanapapswa kufanyika kupitia taasisi zilizoundwa kikatiba.
Ametoa mfano kuwa, ramani ya kuvunjwa Tume Huru ya Uchaguzi IEBC iko wazi kabisa katika katiba na kwamba rais wa nchi na serikali huhusika na kadhia hiyo baada ya mkondo wa bunge kumalizika. Duale ameendelea kusema kuwa vinara wa Cord, Raila Odinga na Kalonzo Musyoka wanaweza kukutana na Rais Uhuru Kenyatta katika Ikulu.
Viongozi wa Cord walihutubia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Nairobi wakati wa kumkaribisha kinara wao Raila Odinga aliporejea kutoka safari ya miezi mitatu Marekani. Katika mkutano huo wakuu wa Cord walitaka mazungumzo ya kitaifa yafanyike ili kujadili changamoto muhimu zinazoikabili Kenya kama vile usalama, ufisadi, uteuzi katika nafasi za umma, mfumo wa uchaguzi na marekebisho katika mfumo wa ugatuzi.

No comments: