Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 3, 2014

'Majenerali wa Nigeria wana uhusiano na Boko Haram'

Majenerali 10 na maafisa wengine watano wa ngazi za juu jeshini nchini Nigeria, wamepandishwa kizimbani katika mahakama za kijeshi kwa tuhuma za kuwa na uhusiano na kundi la kitakfiri la Boko Haram ambalo limekuwa likifanya mashambulizi ya kila mara nchini humo. Gazeti la Leadership la nchini Nigeria limeandika leo kwamba mbali na maafisa hao, maafisa wengine wanne wamepandishwa kizimbani kwa tuhuma za uhaini na kushirikiana na kundi hilo.
Hayo yanajiri wakati ambao, wiki iliyopita Chris Olukolade, Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo alikadhibisha taarifa ya kusailiwa baadhi ya majenerali wa jeshi kwa tuhuma za kushirikiana na Boko Haram. Wanasiasa na hata maafisa wa ngazi za juu jeshini wamekuwa wakiweka bayana kwamba, baadhi ya maafisa wa jeshi wamekuwa wakishirikiana kwa karibu na kundi hilo katika kuendesha operesheni zake za kigaidi. Wakati huo huo familia za wanafunzi wa kike waliotekwa nyara na kundi hilo, wameitaka serikali ya Nigeria kufanya mazungumzo yatakayosaidia kuachiliwa huru wasichana hao. Katika upande mwingine, viongozi wa jimbo la Borno wamesema kuwa, wasichana ambao wiki iliyopita walifanikiwa kutoroka kutoka mikononi mwa wanamgambo wa Boko Haram, wamepelekwa katika shule za Abuja, Lagos na Kaduna ili waendelee na masomo.

No comments: