Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 3, 2014

Saudi Arabia yazuia vitabu vya Ikhwanul Muslimin

Viongozi wa Saudi Arabia wamezuia kuonyeshwa vitabu vya Harakati ya Ikhwaanul Muslimiin katika maonyesho ya vitabu mjini Riyadh. Hayo yamesemwa na Ahmad al-Hamdan, mkuu wa jumuiya ya uchapishaji na usambazaji vitabu ya Saudia, katika maonyesho ya kimataifa ya vitabu ya mwaka 2014 yaliyofunguliwa leo na kuongeza kuwa, kuonyeshwa vitabu vya harakati hiyo katika maonyesho hayo ni hatari kwa usalama wa fikra za kijamii.
Itakumbukwa kuwa siku ya Jumamosi iliyopita, Saudia ilitangaza kuwa, imezuia ushiriki wa jumuiya 350 za uchapishaji na usambazaji vitabu katika nchi za Kiarabu na za kigeni, kutokana na jumuiya hizo kutokuwa na vitabu vinavyoendana na viwango vinavyotakiwa nchini Saudia. Tarehe 7 mwezi Machi mwaka huu, Saudia iliiweka Harakati ya Ikhwaanul Muslimiin katika orodha ya makundi ya kigaidi. Hatua hiyo ilichukuliwa baada ya uungaji mkono wa moja kwa moja wa watawala wa kifalme wa nchi hiyo kwa jeshi lililoongoza mapinduzi dhidi ya Muhammad Mursi wa Misri, rais aliyepinduliwa na jeshi la nchi hiyo. Kabla ya hapo pia na katika kulalamikia uungaji mkono wa Qatar kwa kundi hilo la Ikhwaanul Muslimiin la nchini Misri, tarehe tano mwezi Machi mwaka huu, Saudia, Imarati na Bahrain ziliondoa mabalozi wao mjini Doha, suala ambalo lilitajwa kuwa ni sawa na kutia pilipili kwenye kidonda.

No comments: