Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 3, 2014

Nigeria yakataza maandamano kuhusu wanafunzi

Serikali ya Nigeria imepiga marufuku maandamano yaliyopangwa kufanyika Abuja, mji mkuu wa nchi hiyo kwa lengo la kulalamikia kitendo cha kutekwa nyara wanafunzi wasichana zaidi ya 250 wanaoshikiliwa na kundi la Boko Haram. Taarifa iliyotolewa na polisi imeeleza kuwa, maandamano hayo yamepigwa marufuku kutokana na sababu za kiusalama. Taasisi zilizoratibu maandamano hayo zimeeleza kuwa, zimeshangazwa na uamuzi wa serikali wa kupiga marufuku maandamano hayo, kwa dhana kwamba yatafanyika kwa malengo ya kisiasa.
Hayo yanajiri katika hali ambayo, Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya zimeliweka kundi la Boko Haram kwenye orodha ya makundi ya kigaidi. Inafaa kuashiria hapa kuwa, wanafunzi  hao wa shule ya wasichana ya bweni ya Chibok iliyoko  katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria walitekwa nyara na wanamgambo wa Boko Haram tokea mwezi Aprili, na hadi leo bado wanaendelea kushikiliwa na kundi hilo, licha ya kufanyika  juhudi za kitaifa na kimataifa za kutaka kuwakomboa wanafunzi hao.

No comments: