Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 3, 2014

Larijani: Mashindano ya Qur'ani yameleta nuru nchini

Spika wa Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu wa Iran yaani Bunge amesema kuwa, kuandaliwa mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu kila mwaka mjini Tehran, ni jambo linaloleta nuru na mwanga kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Akizungumza kwenye sherehe za kumalizika duru ya 31 ya mashindano hayo hapo jana, Dakta Ali Larijani amesema kuwa usomaji wa Qur'ani Tukufu una adabu maalumu na kusisitiza kwamba, mwanadamu hawezi kutasawari kupata saada na ufanisi kwa kusoma Qur'ani Tukufu bila ya kuchunga adabu hizo.
Spika wa Bunge la Iran amesema kuwa, Qarii na msomaji Qur'ani Tukufu pia ana daraja maalumu kwa Mwenyezi Mungu, na kwamba daraja hilo huzidi kunyanyuliwa zaidi kila anaposoma Kitabu hicho kitakatifu. Duru ya 31 ya mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu ilimalizika jana, na kwa upande wa qiraa mshindi alikuwa Jaafar Fardi kutoka Iran, na nafasi ya pili hadi ya tano zilishikwa na washiriki kutoka nchi za Ufilipino, Misri, Tajikistan na Tanzania. Na katika upande wa hifdhi, nafasi ya kwanza hadi ya tano zilishikwa na wawakilishi kutoka Iran, Misri, Afghanistan, Indonesia na Niger. Mashindano ya mwaka huu yaliwashirikisha washiriki  98 kutoka nchi 75 duniani na kusimamiwa na majaji 12 kutoka nchi za Kiislamu wakiwemo watano  kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. 

No comments: