Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, June 1, 2014

Msamaha wa masharti wa rais wa Nigeria kwa Boko Haram

Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria ametoa msamaha wa masharti kwa kundi la Boko Haram linalofanya utekaji nyara na mauaji dhidi ya watu wasio na hatia nchini humo. Amesema wanachama wa kundi hilo watasamehewa tu iwapo wataamua kuweka chini silaha zao. Huku akiashiria msamaha uliotolewa na serikali kwa waasi wa kundi la Harakati ya Ukombozi wa Niger Delta baada ya wao kuamua kuweka chini silaha, msemaji wa serikali ya Abuja amewataka Boko Haram watumie fursa iliyotolewa na serikali kwa ajili ya kupata msamaha kama huo.
Kabla ya kupata msamaha, waasi wa Niger Delta kwa miaka mingi walivuruga amani na usalama wa eneo hilo tajiri kwa mafuta kwa kuendesha operesheni za uharibifu. Msamaha wa masharti kwa kundi la Boko Haram umetangazwa ikiwa yamepita masaa machache tu baada ya Rais Jonathan kutoa amri ya kuanzishwa operesheni kubwa ya kupambana na kindi hilo la kigaidi. Boko Haram ni kundi ambalo tokea mwaka 2003 limekuwa likivuruga usalama wa eneo la kaskazini mwa Nigeria kwa kuendesha shughuli za ghasia, mauji na utekaji nyara. Kundi hilo ambalo limeiga misimamo na itikadi za kundi la Taliban la nchini Afghanistan, limekuwa likifuata misimamo mikali na hata kuwakufurisha kirahisi wapinzani wao. Vitendo haribifu vya kundi hilo vilifikia kilele mwezi Aprili uliopita kwa kuwateka nyara wanafunzi wa kike zaidi ya 200 katika shule moja ya bweni. Kitendo hicho cha kushtua kiliwashangaza wengi duniani ambapo vyombo vya habari vya nchi za Magharibi vilitumia vibaya na kipropaganda tukio hilo kwa kulitaja kundi hilo la kigaidi kuwa ni mwakilishi wa watu wa Nigeria na nembo ya Uislamu. Hii ni katika hali ambayo kundi hilo ambalo linachukiwa nchini Nigeria lina wauasi wachache mno kati ya Waislamu wapatao milioni 80 wa nchi hiyo. Wanaigeria wanaamini kwamba kundi hilo lenye misimamo ya kupindukia mipaka linaharibu jina zuri la Uislamu na kuwafanya watu wasio Waislamu kuichukia dini hii tukufu. Wajuzi wengi wa mambo wanaamini kwamba kundi hilo linatokana na njama za kimataifa na kwamba limeundwa na mashirika ya kijasusi ya nchi za Magharibi kwa lengo la kuharibu jina la Uislamu. Katika kuthibitisha madai yao, wataalamu hao wanatolea mfano vitendo vya uhalifu vya kundi hilo vya kuwateka nyara wanafunzi wa kike katika shule za Nigeria na vitendo kama hivyo vinavyofanywa na makundi ya Taliban ya Afghanistan na Pakistan. Wachambuzi wa mambo wanasema kuwa madola ya Magharibi yanaitazama Ngeria kwa jicho la tamaa ya kikoloni kutokana na kuwa ni mojawapo ya nchi ambazo zina utajiri mkubwa wa maliasili katika bara la Afrika. Kwa msingi huo yanafanya njama ya kuzusha migogoro nchini humo ili kuandaa uwanja wa kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo kwa maslahi yao yenyewe. Ni kwa kuzingatia ukweli huo ndipo wakasema kuwa itakuwa vigumu kwa kundi la Boko Haram kukubali kuweka chini silaha zake na msamaha wa masharti uliotolewa hivi karibuni na Rais Goodluck Jonathan wa nchi hiyo. Wataalamu wengine wanasema kuwa kutolewa kwa wakati mmoja amri ya kupambana na Boko Haram na wakati huohuo pendekezo la msamaha kwao ni ishara ya wazi kwamba serikali imeshindwa kulidhibiti kundi hilo. Kundi jingine la wajuzi wa mambo ya Nigeria linadai kuwepo njama ya kuigawa Nigeria katika sehemu mbili kama ilivyofanyika huko Sudan ambapo nchi hiyo iligawanywa na Wamagharibi katika sehemu mbili za kaskazini na kusini

No comments: