Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel
ameikosoa vikali misimamo ya Umoja wa Ulaya ya kuunga mkono makubaliano
yaliyofikiwa baina ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina
'Hamas' na ile ya Fat-h huko Palestina ya kuunda serikali ya umoja wa
kitaifa. Taarifa zinasema kuwa, Kamati ya Usalama ya Israel jana ilimpa
Netanyahu jukumu la kuandaa vikwazo vipya dhidi ya Mamlaka ya Ndani ya
Palestina. Inafaa kuashiria hapa kuwa, siku ya Jumapili iliyopita,
Waziri Mkuu wa Israel alidai kwamba Hamas ni harakati inayotaka utawala
wa Israel utokomezwe, na hivyo kuitaka jamii ya kimataifa kutoitambua
rasmi serikali itakayoshirikishwa harakati hiyo.
Hii ni katika hali
ambayo, mawaziri wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Palestina
waliapishwa jana huko Ramallah, Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment