Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 12, 2014

Israel: Hizbullah ni jeshi la saba kwa nguvu duniani

Mkuu wa jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel, Jenerali Benny Gantz amekiri kuwa, hivi sasa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah nchini Lebanon, ni jeshi la saba kwa nguvu duniani ambapo inamiliki makombora ambayo yanaweza kuyafunika maeneo yote ya utawala huo. Akiashiria uwezo wa harakati hiyo dhidi ya utawala wa Kizayuni, Gantz amesema kuwa, uwezo wa nguvu za Hizbullah unazizidi nchi nyingi zilizoendelea duniani.

Jenerali Benny Gantz ameyasema hayo katika kikao cha mwaka cha Herzliya ambacho kinawakutanisha wakuu wa kisiasa na usalama wa utawala huo bandia ambapo alisema kama ninavyomnukuu: "Nitajieni majina manne au matano ya nchi kubwa zenye uwezo wa kijeshi kama iliyonayo harakati ya Hizbullah huwezi kuzikuta isipokuwa ni Marekani, China, Russia, Ufaransa na Israel." Mwisho wa kunukuu. Ameongeza kuwa, hivi sasa Hizbullah inaendesha mapambano katika pande tatu tofauti na kwamba kuna uwezekano wa kushinda kwa uzoefu wake.
Hata hivyo Jenerali Gantz hakuweka wazi ni mapambano gani hayo matatu yanayoendeshwa na Harakati hiyo ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah nchini Lebanon. Itakumbukwa kuwa, mwaka jana afisa huyo wa jeshi la utawala haramu wa Kizayuni alionya kwamba hatua ya wapiganaji wa Hizbullah kushiriki katika vita nchini Syria, inawaongezea uwezo wa hali ya juu na uzoefu wa kijeshi wapiganaji hao wa harakati hiyo dhidi ya utawala huo wa Kizayuni.

No comments: