Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 12, 2014

Makundi ya kigaidi na kitakfiri yameenea barani Afrika

Gazeti la Daily Telegraph linalochapishwa nchini Uingereza limeandika ripoti inayoonyesha kupanuka satua na wigo wa makundi ya kigaidi barani Afrika. Ripoti hiyo iliyochapishwa kwenye toleo la leo Alhamisi inasema kuwa, makundi ya kitakfiri na yale yenye misimamo ya kufurutu ada ambayo yana mfungamano na mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda yameendelea kuenea kwa kasi na kuwa na ushawishi mkubwa barani Afrika.
"Tangu kuuawa Osama bin Laden mwaka 2011, matawi ya al-Qaeda yamepungua mno katika Peninsula ya Arabia na yanaonekana kuhamia barani Afrika" inasema sehemu moja ya ripoti hiyo. Daily Telegraph limetaja makundi kama vile, al-Shabab la nchini Somalia, Boko Haram la nchini Nigeria na AQIM katika nchi za Algeria, Mali na Niger na kusema kuwa, udhaifu wa serikali za Afrika umetoa mwanya kwa makundi hayo kuendesha harakati zao bila woga.
Huku hayo yakijiri, Serikali ya Uingereza imetahadharisha kwamba, kuna uwezekano wa kushambuliwa Djibouti na kundi la kigaidi la al-Shabab la nchini Somalia. Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza huku ikiashiria kuwa taarifa za kiintelijensia ilizopata kuhusu mipango ya al-Shabab ni za kweli, imewataka raia wake walioko Djibouti kuondoka nchini humo au kuchukua tahadhari ya hali ya juu.

No comments: