Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 12, 2014

ICRC laonya juu ya hali ya kibinadamu Sudan Kusini

Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu, limeonya juu ya hali mbaya ya kibinaadamu nchini Sudan Kusini. Shirika hilo lenye makao yake mjini Geneva, sambamba na kutoa ripoti kuhusiana na suala hilo limesema kuwa, hali ya kibinaadamu nchini humo ni ya hatari na kuongeza kuwa, hali imekuwa mbaya zaidi katika kipindi hiki kufuatia kuanza kunyesha kwa mvua ambazo kwa mujibu wa shirika hilo, zitakwamisha zoezi la kufikisha misaada ya kibinaadamu kwa waathirika wa mgogoro nchini humo.

Aidha shirika hilo limesisitiza kuwa, tangu kuanza kwa mgogoro nchini Sudan Kusini mwezi Disemba mwaka jana, zaidi ya watu laki mbili na elfu 50 wameshapokea misaada ya shirika hilo. Wakati huo huo mkuu wa timu ya shirika la Msalaba Mwekundu nchini Sudan Kusini amesema kuwa, hadi sasa hali ya mambo nchini humo bado ni mbaya na kwamba, ikiwa misaada haitawafikia wahusika haraka, basi kuna uwezekano wa kuongezeka uhaba wa chakula ndani ya nchi hiyo changa zaidi barani Afrika.
Kwa upande mwingine Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu, limezitaka pande zinazopigana nchini Sudan Kusini kutekeleza ahadi zao kwa mujibu wa sheria za kimataifa ili kuiepusha nchi hiyo na umwagikaji damu zaidi.

No comments: