Chama tawala nchini Ivory Coast kimekaribisha uamuzi wa kuhukumiwa rais
wa zamani wan chi hiyo Laurent Gbagbo katika Mahakama ya Kimataifa ya
Jinai ICC. Msemaji wa chama hicho Joël N'guessan aliwambia wanachama wa
chama hicho hapo jana kuwa, chama tawala kinakubaliana na tuhuma
zinazomkabili Gbagbo katika mahakama hiyo na kwamba hatua hiyo itasaidia
kuleta usalama nchini humo.
Aidha Joël ameunga mkono uamzi wa ICC wa
kukubaliana na tuhuma za jinai dhidi ya binaadamu zinazomkabili
mtuhumiwa huyo, na kwamba hatua hiyo italeta furaha kwa familia za
wahanga wa matukio ya baada ya uchaguzi wa mwaka 2010 nchini humo. Siku
ya Alkhamis Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ilikubali kuakhirisha
kesi ya rais wa zamani wa Kodivaa, Laurent Gbagbo hadi Agosti 13 mwaka
huu iliyokuwa imepangiwa kuanza Juni 18 lakini mawakili wa Gbagbo
wakasema mteja wao hawezi kuhudhuria vikao vya kesi hiyo kutokana na
hali yake mbaya ya kiafya kwa sasa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment