Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, May 23, 2014

UN yaonya tena juu ya mgogoro wa chakula S/Kusini

Kwa mara nyingine tena Umoja wa Mataifa umeonya kuhusiana na mgogoro wa chakula nchini Sudan Kusini. Toby Lanzer, Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya misaada ya kibinadamu nchini humo amesema kuwa, hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu mgogoro wa vita unaoendelea Sudan Kusini utawasababishia janga la njaa zaidi ya thuluthi moja ya wananchi wa nchi hiyo changa zaidi barani Afrika. Lanzer ameongeza kuwa, kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa, karibu watu milioni moja na laki tano ambao wako katika hatari ya kuyakimbia makazi yao, watu laki nane na 50 elfu ambao ni wakimbizi na wengine milioni nne kwa pamoja wanakabiliwa na tishio la uhaba mkubwa wa chakula.
Lanzer ameyasema hayo nchini Norway katika kikao cha wafadhili wa kimataifa kwa ajili ya nchi hiyo. Washiriki wa mkutano huo wameahidi kuchangia dola milioni 600 kwa ajili ya kukabiliana na ukame Sudan Kusini. Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia masuala ya misaada ya kibinaadamu Bi. Valerie Amos amesisitiza kuwa, haifai kucheleweshwa suala hilo na kusubiri kuharibika zaidi hali ya mambo, bali kuna udharura wa kumalizwa tatizo hilo haraka iwezekanavyo.

No comments: