Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, May 22, 2014

Russia itapigia veto azimio la kushtakiwa Syria ICC

Balozi wa Russia katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa nchi yake itapigia kura ya turufu azimio la kutaka kushitakiwa Syria katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC).
Vitaly Churkin amesema azimio hilo lililopendekezwa na Ufaransa na ambalo linatarajiwa kupigiwa kura leo, litarudisha nyuma jitihada za kuutafutia suluhisho la kisiasa mgogoro wa Syria.
Azimio hilo linavituhumu vikosi vya serikali, wanamgambo wanaounga mkono serikali na waasi wanaopigana dhidi ya serikali ya Damascus kufanya mauaji.

Jana mwakilishi wa Syria katika Umoja wa Mataifa Bashar al Jaafari alizitaka nchi za dunia kutounga mkono azimio hilo akisema kuwa, azimio hilo ni la upendeleo na lengo lake ni kuzuia fursa ya kutatuliwa mgogoro wa nchi hiyo kwa njia za amani.

No comments: