Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, December 25, 2013

UN kutuma vikosi zaidi nchini Sudan Kusini

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumanne hii liliidhinisha mipango ya kuongeza karibu mara mbili idadi ya askari jeshi wa kulinda amani huko Sudan Kusini katika juhudi za kuwalinda raia na machafuko huku taarifa za kugunduliwa makaburi ya umati zikizusha hofu ya kutokea mapigano ya kikabila katika taifa hilo changa zaidi duniani.  Baraza la Usalama limesema limeidhinisha kutumwa huko Sudan Kusini wanajeshi wengine elfu sita.

Nchi 15 wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa jana ziliidhinisha kwa sauti moja mpango wa Ban Ki-moon Katibu Mkuu wa umoja huo wa kuimarisha nguvu za kikosi cha wanajeshi wa kulinda amani huko Sudan Kusini kwa kuzidisha idadi ya wanajeshi hadi 12,500 na polisi 1323. Umoja wa Mataifa unaongeza kiwango hicho cha walinda amani huko Sudan Kusini huku raia wa nchi hiyo wasiopungua elfu 45 wakiwa wamepata hifadhi katika vituo vya umoja huo. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa hata hivyo ametahadharisha kuwa walinda amani hao hawataweza kumlinda kila raia anayehitaji msaada huko Sudan Kusini licha ya kuongezwa kwa idadi hiyo ya askari wa kulinda amani. 

No comments: