Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 8, 2013

Watu 16 wauawa kwenye machafuko ya Misri

Kwa akali watu 16 wameuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa, baada ya waandamanaji wanaomuunga mkono Muhammad Morsi rais aliyeondolewa madarakani nchini Misri kupambana na askari wa usalama wa nchi hiyo. Harakati ya Ikhwaanul Muslimiin imetangaza kuwa, wafuasi hao wa Mosri wameuawa mapema leo wakati walipokuwa wakifanya maandamano ya kupinga kuondolewa madarakani Muhammad Morsi.
Ahmad Aref Msemaji wa Ikhwanul Muslimiin amesema kuwa, wafuasi hao wa Morsi wameuawa baada ya kufyatuliwa risasi na askari wa usalama na mamia ya wengine kujeruhiwa, baadhi yao hali zao zimeripoti kuwa mahututi. Wakati huohuo, Muhammad Morsi rais aliyondolewa madarakani pamoja na viongozi wengine wanane wa ngazi za juu wa Ikhwanul Muslimiin wataanza kuhojiwa leo kwa tuhuma za kuvivunjia heshima vyombo vya sheria vya nchi hiyo. Shakhsia hao pia wamepigwa marufuku kufanya safari nje ya nchi hiyo.

No comments: