Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 8, 2013

Tsvangirai amkosoa vikali Rais Mugabe wa Zimbabwe

Morgan Tsvangirai Waziri Mkuu wa Zimbabwe amemkosoa vikali Rais Robert Mugabe wa nchi hiyo kwa kushindwa kutekeleza marekebisho ya kidemokrasia nchini humo. Akihutubia kwenye mkutano wa kampeni, Tsvangirai ambaye pia ni  kiongozi wa chama cha MDC amesema kuwa, inashangaza kuona kwamba zimeanza kampeni za uchaguzi kabla ya kufanyika marekebisho muhimu ya demokrasia nchini humo. Waziri Mkuu wa Zimbabwe ambaye ni hasimu mkubwa wa kisiasa wa Rais Mugabe amesisitiza kuwa, atashiriki kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi ujao wa rais, ijapokuwa marekebisho hayo yangesaidia uchaguzi huo kuwa huru na wa haki.
Imepangwa kuwa, uchaguzi wa rais na bunge nchini Zimbabwe utafanyika Julai 31 mwaka huu. Inafaa kuashiria hapa kuwa,  Jumuiya ya Ustawi ya Kusini mwa Afrika SADC ilimshinikiza Rais Mugabe na kumtaka aitishe uchaguzi baada ya wiki mbili tokea tarehe iliyopangwa awali, lakini Mahakama ya Katiba ya nchi hiyo ilipinga takwa hilo na kusisitiza juu ya kufanyika uchaguzi huo katika tarehe iliyopangwa awali, yaani Julai 31 mwaka huu.

No comments: