Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, July 6, 2013

Viongozi wa Amerika ya Latini wazilaani nchi za EU

Marais wa nchi za Amerika ya Latini wamelaani hatua ya nchi kadhaa za Ulaya ya kuzuia ndege ya Rais Evo Morales wa Bolivia kupaa kwenye anga ya nchi zao na hivyo kuhatarisha maisha ya kiongozi huyo.
Marais wa Venezuela, Ecuador, Argentina, Uruguay na Suriname wamesema Marekani ndiyo inayopaswa kulaumiwa kwani hakuna shaka kwamba nchi zilizozuia ndege ya Morales zilipata mashinikizo kutoka Washington.

Rais Evo Morales alikuwa akitoka Russia baada ya kuhudhuria mkutano wa kimataifa wa nishati na ndege yake ililazimika kutua kwa dharura nchini Austria baada ya Ufaransa, Uhispania na Ureno kukataa kuiruhusu ndege hiyo ipae kwenye anga yao.
Taarifa ya pamoja ya viongozi hao imetaka maelezo ya haraka kutoka nchi hizo tatu za Ulaya kuhusiana na tukio hilo huku wakisema hatua hiyo ya Paris, Lisbon na Madrid ni ukiukaji wa sheria za kimataifa. Rais wa Bolivia ametishia kufunga ubalozi wa Marekani akisema Washington haina heshima kwa mtu yeyote.

No comments: