Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 8, 2013

Umoja wa Ulaya walaani mauaji ya wanafunzi Nigeria

Umoja wa Ulaya umelaani vikali mauaji ya kikatili dhidi ya wanafunzi wa shule moja ya sekondari ya bweni nchini Nigeria. Mkuu wa Siasa za Nje za Umoja wa Ulaya sambamba na kulaani mauaji hayo ametaka magaidi waliofanya jinai hiyo kufuatiliwa kisheria. Bi Catherine Ashton amesema, Umoja wa Ulaya unalaani mauaji ya wanafunzi 28 na mwalimu mmoja huko Nigeria yaliyofanywa na kundi la Boko Haram na unaitaka serikali ya Nigeria ihakikishe waliofanya jinai hiyo wanaadhibiwa kisheria.

Siku chache zilizopita, watu wenye silaha waliishambulia  na kuichoma moto shule moja kaskazini mashariki mwa Nigeria na kuuwa wanafunzi 28 na mwalimu mmoja wa shule hiyo. Wakati huo huo, viongozi wa Nigeria wametangaza kufungwa shule za sekondari katika jimbo la Yobe kufuatia mauaji ya wanafunzi  wa shule ya msingi yaliyofanywa siku ya Jumamosi.

No comments: