Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 8, 2013

Jumatatu, Julai 8, 2013

Leo ni Jumatatu tarehe 29 Shaaban 1434 sawa na Julai 8, 2013.
Siku kama ya leo miaka 19 iliyopita, alifariki dunia Kim Il-sung aliyekuwa Kiongozi na Katibu Mkuu wa Chama cha Kikomonisti wa Korea Kaskazini. Kim Il-sung alizaliwa mwaka 1912. Akiwa na cheo cha ukapteni jeshini alirejea kaskazini mwa nchi hiyo mwaka 1945 akiandamana na jeshi. Alipanda ngazi ya uongozi haraka na akachaguliwa kuwa kiongozi wa chama cha wakomunisti wa nchi hiyo. Mwaka 1948 wakati nchi hiyo ilipoasisiwa na kuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea Kim Il-sung alifikia cheo cha uwaziri mkuu. Katika vita vya Korea Kim Il-sung aliteuliwa kuwa kamanda mkuu wa majeshi ya nchi hiyo na mwaka 1972 akawa rais wa taifa hilo.

Miaka 57 iliyopita katika siku kama hii ya leo alifariki dunia mtaalamu, mwanafikra na mwandishi wa Kitaliano Giovanni Papini. Alizaliwa mwaka 1881 katika mji wa Florence nchini Italia. Giovanni alipitia kipindi kigumu cha utoto na ujana wake. Hata hivyo hamu yake kubwa ya masomo ilimpelekea kwenda katika maktaba za kijamii na kuzidisha elimu na taratibu alidhihirisha uwezo wake mkubwa katika taaluma ya fasihi. Msomi huyu ameandika vitabu vingi kama "A man--finished," "The Failure," na “Life of Christ,"
Na siku kama ya leo miaka 1215 iliyopita alifariki dunia faqihi, mtaalamu wa hadithi na mpokezi wa matukio ya kihistoria maarufu kwa jina la Abu Naiim. Alizaliwa mwaka 130 Hijria nchini Iraq na anatambulika kama mpokezi anayetegemewa na kuheshimiwa na maulamaa wa Kiislamu wa hadithi. Ameandika kitabu cha As Salaat, na mwanahistoria maarufu Ibn Nadim anasema kuwa, msomi huyo ameandika pia vitabu vya “al Manasik” na “Masailul Fiqhi”.

No comments: