Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, July 9, 2013

Rais wa Namibia ataka kuimarishwa uhusiano na Iran

Rais wa Namibia ameeleza matarajio yake ya kustawishwa uhusiano wa nchi yake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Akizungumza hii leo huko Namibia na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Ali Akbar Salehi, Rais Hifikepunye Pohamba wa Namibia amepongeza uchaguzi wa rais nchini Iran na kueleza kuwa, matokeo na namna duru ya 11 ya uchaguzi wa rais wa Iran ulivyoendeshwa vinaonyesha jinsi wananchi wa Iran wanavyounga mkono demokrasia. Rais wa Namibia meashiria uhusiano wa kihistoria wa wananchi wa Namibia kupitia ofisi ya Swapo hapa mjini Tehran na kueleza kuwa Iran ilidhihirisha urafiki wake wa kweli na Namibia kwa kufungua ofisi ya harakati ya Swapo kabla ya uhuru wa nchi hiyo na kuendelezwa mahusiano kati ya nchi mbili hizi hata baada ya Namibia kupata uhuru.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameashiria irada ya viongozi wa ngazi ya juu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya kutaka kuwa na uhusiano mzuri na Namibia na kueleza kuwa Iran imepata mafanikio na maendeleo makubwa katika nyuga mbalimbali katika kipindi cha miaka 34 iliyopita na sasa iko tayari kutoa uzoefu na utaalamu wake huo kwa nchi nyingine rafiki ikiwemo Namibia.        

No comments: