Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, July 9, 2013

Kethi Kilonzo afungiwa kushiriki uchaguzi mdogo Kenya

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya IEBC imemzuia Bi. Kethi Kilonzo, mwana wa kike wa waziri wa zamani nchini humo kuwania kiti cha Seneta kwenye jimbo la Makueni baada ya kubainika kuwa, hajatimiza masharti ya kugombea nafasi hiyo.
Jopo lililoundwa na IEBC kufuatilia kadhia hiyo limetoa uamuzi likisema Bi. Kilonzo hajajiandikisha kama mpiga kura na hivyo hawezi kugombea wadhifa huo. Kiti cha useneta cha Makueni kiliachwa wazi baada ya kufariki dunia Mutula Kilonzo, baba yake Kethi Kilonzo, takriban miezi miwili iliyopita.
Kethi alikuwa amepania kuwania kiti hicho kwa muungano wa CORD unaoongozwa na waziri mkuu wa zamani Raila Odinga. Hata hivyo muungano huo umesema utapinga uamuzi huo wa IEBC katika Mahakama Kuu na umesisitiza kwamba, Kethi ametimiza masharti yote ya kupiga kura na hata kuwania wadhifa wowote wa uchaguzi.
Mbali na Bi Kilonzo, jopo la IEBC lilikuwa linamchunguza mgombea wa muungano wa Jubilee ambapo limeamua kuwa, Bw. Philip Kaloki ametimiza masharti yote na anaweza kugombea kwenye uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu.  

No comments: