Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, July 9, 2013

Mashirika ya ujasusi ya kigeni yanayasaidia makundi ya ukufurishaji

Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran yaani Bunge Dakta Ali Larijani amesema kuwa mashirika ya ujasusi ya nchi za nje yanayaunga mkono makundi ya wanamgambo wanaowakufurisha Waislamu wengine katika nchi za Kiislamu ikiwemo Misri. Larijani amesema mkono wa mashirika hayo ya ujasusi umeshuhudiwa katika nchi mbalimbali zikiwemo Iraq, Afghanistan na Misri. Ameongeza kuwa makundi hayo yanayowakufurisha Waislamu wengine daima yamekuwa balaa kubwa kwa Uislamu.
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amesema makundi hayo yanadai kuwa yanafanya Jihad na akahoji ni Jihadi gani hiyo inayoruhusu kuua Waislamu. Ali Larijani amesema baadhi ya serikali za Magharibi zimekutana na makundi hayo yenye kufurutu ada huko Iraq na kuyaahidi kuyaunga mkono katika mapambano yake dhidi ya Waislamu wa madhehebu ya Shia na Jamhuri ya Kiislamu.  

No comments: