Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 10, 2013

Jalili: Marekani haiaminiki

Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Saeed Jalili amesema kuwa, Marekani si nchi ya kuaminika na haifai kufanya ushirika nayo. Jalili ameyasema hayo leo hapa mjini Tehran alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Afghanistan, Ershad Ahmadi kuhusu uhusiano wa pande mbili. Jalili ameongeza kuwa, 'sera za kigeni za Marekani katika eneo hili ni ishara ya wazi kuwa Washington inapinga umoja, uthabiti na ustawi wa nchi za Kiislamu.' Amesema imeibainikia jamii ya kimatiafa hasa watu wa eneo kutoka Afghanistan hadi Misri kuwa, madai ya Marekani ya kupambana na ugaidi na kuunga mkono demokrasia ni uongo mtupu.'
Afisa huyo wa Iran amesema kuwa, 'kuunga mkono ugaidi na kupinga demokrasia ndio msingi wa sera za Marekani katika eneo hili.'
Jalili pia amesema, kuna haja ya kuimarisha uhusiano wa Iran na Afghanistan. Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Afghanistan ameipongeza serikali ya Iran kwa kuendelea kuwasaidia watu wa Afghanistan katika kipindi chote cha masaibu nchini humo. Ameelezea matumaini yake kuwa uhusiano wa Tehran na Kabul utaimarika zaidi baada ya vikosi vya nchi za Magharibi kuondoka kabisa katika eneo hili. Ikumbukwe kuwa Marekani na waitifaki wake waliivamia Afghanistan mwaka 2001 katika kile kilichodaiwa kuwa eti ni vita dhidi ya ugaidi. Hata hivyo hadi leo Afghanistan bado imesakamwa na jinamizi la ugaidi.

No comments: