Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 10, 2013

MNLA yatuhumiwa kuvuruga amani Mali

Jeshi la Mali limeituhumu harakati ya Azawad MNLA kwa kukiuka makubaliano ya amani yaliyofikiwa nchini Burkina Faso.
Kanali Diarran Kone kutoka Jeshi la Mali amesema kuwa, harakati ya Azawad tangu Jumamosi iliyopita imekuwa ikiwakusanya wanawake na watoto wa eneo la Kidal, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo na kuwashambulia wanajeshi wa Mali na askari wa kulinda amani kutoka nchi za Kiafrika. Amesema kuwa, harakati hiyo iliwashawishi wananchi wa eneo la Kidal kufanya maandamano wakati yalipoingia majeshi ya kulinda amani ya Kiafrika MINUSMA na kujeruhi wanajeshi kadhaa. Wanajeshi 150 wa Mali Ijumaa iliyopita waliingia kwenye mji wa Kidal, baada ya kufikiwa makubaliano ya amani ya pande hizo mbili Juni 18 nchini Burkina Faso.

No comments: