Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 10, 2013

Adly Mansour atangaza tarehe ya uchaguzi Misri

Rais wa serikali ya mpito ya Misri Adly Mansour ametangaza kwamba uchaguzi wa bunge nchini humo utafanyika mwaka 2014.
Rais Mansour ameongeza kuwa, mara baada ya kufanyika uchaguzi wa bunge, itatangazwa tarehe ya kufanyika uchaguzi wa rais. Rais wa serikali ya mpito ya Misri ana kipindi cha miezi sita cha kuifanyia marekebisho katiba ya nchi hiyo ambayo hivi sasa imesitishwa.

Wakati huohuo, Msemaji wa Rais wa serikali ya mpito wa Misri amesema kuwa, matukio yaliyojiri jana mjini Cairo hayawezi kuzuia uundwaji wa serikali mpya. Ahmad al Musalmani amesema kuwa, mapigano yaliyotokea jana kati ya wafuasi wa Harakati ya Ikhwanul Muslimiin na vikosi vya usalama mbele ya makao ya Gadi ya Rais mashariki mwa Cairo, hayawezi kuzuia juhudi za kuundwa serikali mpya  au kutekelezwa mpango wa ramani ya njia uliobuniwa na jeshi la nchi hiyo. Zaidi ya watu 50 waliuawa kwenye mapigano ya jana na mamia ya wengine kujeruhiwa.

No comments: