Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 10, 2013

Mkakati wa Sudan na Chad wa kuwakamata wahalifu

Serikali ya Sudan na Chad kwa pamoja zimeamua kushirikiana kwa minajili ya kuwatia mbaroni watu waliohusika wa mauaji ya Mkuu wa Harakati ya Uadilifu na Usawa na msaidizi wake ndani ya mipaka ya ardhi ya Chad.
Yassir Ahmad Muhammad, Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Jinai ya Darfur amesema kuwa, zoezi la kuwasaka watu waliohusika na jinai ya kumuua Muhammad Bashar AbdulRahman mkuu wa harakati hiyo na msaidizi wake limekwishaanza.
Amesema kuwa, hadi sasa idara  ya upepelezi ya  Sudan inawatuhumu  watu 18 kwa kuhusika na mauaji hayo na kusisitiza kwamba, tukio hilo limepangwa kwa lengo la kuzusha ghasia na machafuko zaidi katika jimbo la Darfur.
Inafaa kuashiria hapa kuwa, mwezi uliopita  Muhammad Bashar akiwa pamoja na msaidizi wake waliuawa ndani ya mpaka wa Chad, shambulio lililofanywa na waasi wanaofungamana na kundi la Uadilifu na Usawa tawi la Jibril Ibrahim.

No comments: