Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA unatarajiwa kufanya
duru mpya ya mazungumzo na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mwezi ujao wa
Agosti.
Mazungumzo hayo yatajadili kwa kina kadhia ya Nyuklia ya Iran ambapo
mwanadiplomasia mmoja wa wakala huo amesema kwamba, kuna matumaini ya
kufikiwa makubaliano ya kiwango fulani.
Mwanadiplomasia huyo ambaye
hakutaka jina lake litajwe amedai kuwa, kwa kuzingatia kwamba mazungumzo
hayo yatakuwa ya kwanza tangu baada ya uchaguzi wa rais wa mwezi Juni,
huenda serikali mpya ya Rais mteule Hassan Rohani ikawa na misimamo ya
wastani kwenye mazungumzo ikilinganishwa na serikali inayoondoka ya Rais
Mahmoud Ahmadinejad.
Dkt. Rohani anafahamika kwa misimamo yake ya wastani na wengi katika
ulimwengu wa Magharibi wamempa jina la 'Sheikh Mwanadiplomasia.'
No comments:
Post a Comment