Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 29, 2013

Watu 48 wauawa katika mapigano ya kikabila Nigeria

Watu wasiopungua 48 wameuawa na nyumba nyingi kuteketezwa moto kufuatia mapigano ya kikabila katika eneo la kati mwa Nigeria.
Msemaji wa Jeshi la Nigeria katika jimbo la kati la Plateau Kapteni Salisu Mustapha amesema kati ya waliopoteza maisha ni wakaazi 28 wa kijiji cha Langtang na wavamizi 20 ambao waliuawa na wanajeshi walioitwa kutuliza hali ya mambo.
Viongozi wa kijamii wanasema machafuko hayo ya Alkhamisi yaliibuka kufuatia msururu wa wizi wa mifugo katika jimbo hilo.  Wanakijiji wengi wanaripotiwa kukimbia makaazi yao kwa kuhofia machafuko zaidi baina ya makabila hasimu ya Fulani na Tarok. Maelfu ya Wanigeria wamepoteza maisha katika mapigano ya kikabila katika eneo la kati mwa nchi hiyo. Aidha eneo la kaskazini mwa Nigeria pia limeshuhudia machafuko katika miaka ya hivi karibuni ambapo maelfu ya watu pia wamepoteza maisha kufuatia uasi wa kundi la Boko Haram.

No comments: