Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 29, 2013

Ban: Afrika ni bara linalopiga hatua kimaendeleo

Ban Ki moon Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelitaja bara la Afrika kuwa ni bara lenye kupiga hatua kimaendeleo. Akizungumza na vyombo vya habari mjini New York, Ban Ki moon amesema kuwa nchi nyingi za Kiafrika zimefanikiwa katika kuleta amani, kupunguza kiwango cha umasikini, kuongeza kipato cha wananchi na kupiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya maradhi hatari, kama vile malaria na ukimwi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameongeza kuwa, Waafrika wameweka azma ya kuimarisha demokrasia, na hali kadhalika kupambana na vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu na ufisadi. Hata hivyo, Ban Ki moon amesisitiza kuwa, nchi za Kiafrika bado zinakabiliwa na changamoto nyingi, hivyo amewataka viongozi na Waafrika kwa ujumla kupiga hatua zaidi ili kukabiliana na changamoto hizo.

No comments: