Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 29, 2013

Machafuko makubwa Misri, Mursi atoroka Cairo

Ijumaa hii kumeshuhudiwa maandamano makubwa katika mji mkuu wa Misri, Cairo baina ya wafuasi na wapinzani wa rais Mohammad Mursi.
Wafuasi wa Mursi walikusanyika nje ya msikiti mkubwa wa eneo la Nasr huku wapinzani wakikutana katika Medani ya Tahrir. Wakiwa hapo wakijaribu bila mafanikio kuandamana hadi katika Ikulu ya Rais.

Baadhi ya duru za habari zinaarifu kuwa Rais Mohammad Mursi ameukimbia mji wa Cairo na kuenda eneo lisilojulikana. Aidha imearifiwa kubwa Ubalozi wa Marekani mjini Cairo utafungwa kwa siku kadhaa kwa kuhofia hujuma ya waandamanaji.
Wapinzani nchini Misri wameitisha maandamano makubwa kote nchini humo Juni 30 ambapo wanataka kumlazimisha Rais Mursi ajiuzulu. Wanamlaumu kiongozi huyo kuwa amekengeuka mkondo wa mapinduzi yaliyomtimua madarakani dikteta Hosni Mubarak. Uamuzi wa Mursi wa kukata uhusiano na Syria na kuwaunga mkono magaidi nchini humo pia ni jambo ambalo limewakasirisha wananchi wa Misri.

No comments: