Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 28, 2013

Wapinzani Misri wakataa mazungumzo na serikali

Muungano wa wapinzani nchini Misri NSF umetangaza wazi kwamba hauna nia ya kufanya mazungumzo na Rais Muhammad Morsi na umekosoa vikali hotuba ya kiongozi huyo aliyoitoa kwa mnasaba wa sherehe za kukumbuka mwaka mmoja tangu alipoingia madarakani.
Wapinzani hao wamesisitiza juu ya kufanyika maandamano makubwa tarehe 30 mwezi huu dhidi ya rais huyo. Mbali na mrengo huo kusisitizia kufanya maandamano hayo ya siku ya Jumapili, pia umemtaka Rais Morsi ajiuzulu na kutoa fursa ya kufanyika uchaguzi wa mapema.
Msemaji wa kambi hiyo Bwana Khalid Daud amekosoa tuhuma zilizotolewa na Rais Morsi na kusema hazina msingi wowote. Daud ameongeza kuwa, viongozi wa kambi hiyo nao watashiriki katika maandamano ya siku ya Jumapili.
Wakati huo huo jumuiya ya Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Misri, imelaani vikali mauaji ya kikatili yaliyofanywa na Masalafi wenye misimamo mikali dhidi ya mwanazuoni maarufu wa Kishia Sheikh Hassan Shehata na wafuasi wake wanne nchini Misri. Viongozi wa jumuiya hiyo wamewaambia wanahabari kuwa, serikali imeshindwa kuwalinda raia wake hususan wafuasi wa madhehebu ya Shia.

No comments: