Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 28, 2013

Milioni 6 kushiriki uchaguzi wa bunge Rwanda

Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Rwanda imetangaza kuwa, takriban watu milioni 6 wanatarajiwa kushiriki kwenye uchaguzi wa bunge uliopangwa kufanyika mwezi Septemba mwaka huu.
Watu milioni 4.8 ndio walioshiriki kwenye uchaguzi wa bunge wa mwaka 2008. Mwenyekiti wa tume hiyo, Prof. Kalisa Mbanda amesema matayarisho yanakaribia kukamilika na kwamba uchaguzi huo utagharimu Faranga bilioni 5.
Amesema kutokana na maafisa wake kupata uzowefu wa kutosha, gharama za zoezi hilo zimepungua ikilinganishwa na mwaka 2008 ambapo fedha zilizotumika zilikuwa Faranga bilioni 9.
Tayari baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani wamerudi Rwanda kutoka nchi za nje kwa ajili ya kuandaa vyama vyao kwa uchaguzi huo. Rais Paul Kagame majuma kadhaa yaliyopita alitoa onyo kali kwa wanasiasa waliorudi nyumbani akisema wale watakaojaribu kutumia mwanya wa kampeni kuwagawa wananchi watakabiliwa na mkono mrefu wa sheria.

No comments: