Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 28, 2013

Ijumaa Juni 28, 2013

Leo ni Ijumaa tarehe 19 Shaaban 1434 Hijria sawa na Juni 28, 2013.
Miaka 1428 iliyopita katika siku inayosadifiana na hii ya leo, vita vya Banil Mustalaq vilitokea. Bani Mustalaq lilikuwa kabila miongoni mwa makabila ya Khaza'ah ambalo lilihamia katika vitongoji vya Makka. Viongozi wa kaumu hiyo walikuwa wakiabudu masanamu na kueneza ibada hiyo huko Makka. Banil Mustalaq walijiandaa kupigana vita na Uislamu baada ya Waislamu kushika madaraka huko Madina. Kwa msingi huo, Mtume Muhammad aliingia vitani pamoja na wafuasi wake kadhaa na kutoa pigo kubwa kwa kabila hilo.
Miaka 32 iliyopita mwafaka na tarehe Saba mwezi Tir mwaka 1360 Hijria Shamsiya, Ayatullah Dakta Muhammad Beheshti aliuawa shahidi akiwa pamoja na watu wengine 72 waliokuwa miongoni mwa shakhsiya bora wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran baada ya kuripuliwa kwa bomu ofisi kuu ya chama cha Jamhuri ya Kiislamu. Ayatullah Beheshti pia alikuwa miongoni mwa shakhsiya wa awali na waliotoa mchango mkubwa katika Mapinduzi ya Kiislamu. Dakta Beheshti pia alikuwa mmoja kati ya wasaidizi wakuu wa Imam Khomeini Mwenyezi Mungu amrehemu. Mlipuko huo wa bomu uliwauwa shahidi Dakta Beheshti na wasaidizi 72 wa Imam Khomeini wakiwemo mawaziri na wabunge kadhaa.
Na siku kama ya leo miaka 7 iliyopita sawa na tarehe 28 mwezi Juni mwaka 2006 jeshi la utawala wa Kizayuni lilianzisha mashambulio makubwa dhidi ya watu wa Ukanda wa Ghaza. Utawala wa Kizayuni uliendesha mashambulio hayo ya kinyama kwa kisingizio cha kuuawa wanajeshi wake wawili siku tatu kabla ya mashambulio hayo. Israel ilidai kuwa wanamapambano wa Palestina walifanya oparesheni katika kituo kimoja cha upekuzi na kuua wanajeshi wake wawili na kumkamata mateka mwingine mmoja. Idadi kadhaa ya mawaziri, wabunge na wawakilishi wa baraza la mji la serikali halali ya Palestina inayoongozwa na Hamas walitekwa nyara na wanajeshi wa Israel katika siku za kwanza za mashambulizi hayo makubwa ya jeshi yaliyopewa jina la "Mvua za Kiangazi". Mbali na hayo, mamia ya raia madhlumu wa Palestina waliuawa shahidi na kujeruhiwa katika mashambulizi ya kinyama ya anga na nchi kavu ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Ghaza.

No comments: