Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 29, 2013

Wakimbizi watishia kujiua Munich, Ujerumani

Watu walioomba hifadhi ya kisiasa katika mji wa Munich nchini Ujerumani na kufanya mgomo wa kula hadi yatakapotekelezwa matakwa yao, wamegoma kulishwa vyakula vya majimaji na wametishia kujiua. Watu hao wanaofikia idadi yao 50 kutoka nchi za Nigeria, Ethiopia, Pakistan na nchi nyingine wamesisitiza kuwa hawatalegeza kamba hadi litakapotekelezwa takwa lao la kupewa hifadhi ya kisiasa  nchini humo.
Timu ya madaktari imeeleza kuwa, kitendo cha wanasiasa hao kukataa kula na kunywa kitahatarisha zaidi maisha yao. Duru za hospitali zinaeleza kuwa, wafanya mgomo 19 wamefikishwa hospitali, akiwemo mama mmoja mwenye watoto wawili baada ya hali zao kuwa mbaya.

No comments: