Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 29, 2013

'Wapinzani hawataweza kumpindua Rais Morsi'

Harakati ya Ikhwaanul Muslimiin nchini Misri imetangaza kuwa haitatoa mwanya wa kupinduliwa utawala wa Rais Muhammad Morsi wa nchi hiyo. Mohammad al Beltagui mbunge na kiongozi mwandamizi wa harakati ya Ikhwanuul Muslimiin amewahutubia maelfu ya wafuasi wa Rais Morsi mjini Cairo na kusisitiza kuwa, harakati hiyo kamwe haitatoa fursa kwa wapinzani kufanya mapinduzi yatakayopelekea kumuondoa madarakani Rais Morsi.
Al Beltagui amesisitiza kuwa, serikali ya Morsi haiwezi kufananishwa na utawala wa Hosni Mubarak dikteta aliyeondolewa madarakani nchini humo, na kuongeza kuwa, wapinzani hawana uwezo wa kutekeleza mapinduzi mengine nchini humo. Duru za habari zinasema kuwa, Rais Morsi pamoja na familia yake ameondoka kwenye Ikulu ya nchi hiyo na kuelekea mahala pasipojulikana, kukwepa maandamano makubwa yatakayofanywa na wapinzani hapo kesho Jumapili  nchini humo.

No comments: