Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 14, 2013

Waandishi habari wa kigeni kuakisi uchaguzi Iran

Mamia ya waandishi habari wa nchi za kigeni tayari wawo hapa nchini kwa ajili ya kuakisi uchaguzi wa rais wa Iran unaofanyika leo Juni 14. Alireza Shirvani Mkuu wa ofisi ya Maripota wa Kigeni ya Wizara ya Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, karibu waandishi habari 430 wanaowakilisha mashirika tofauti ya habari yapatayo 190 kutoka nchi 40 duniani wapo hapa nchini kwa ajili ya kuakisi zoezi la uchaguzi wa rais.
Katika upande mwingine Waziri wa Mambo ya Ndani ya Iran ametangaza kuwa vituo 60 elfu vya kupigia kura nchi nzima viko tayari kwa ajili ya zoezi la uchaguzi wa rais wa Iran na Mabaraza ya Miji na Vijiji unaofanyika leo.
Mustapha Muhammad–Najjar ameeleza kuwa, kura zitaanza kupigwa saa mbili asubuhi leo Ijumaa na zoezi hilo litaendelea kwa masaa 10 hadi saa 12 jioni na kwamba iwapo itahitajika muda utaongezwa kwa mujibu wa sheria.  Muhammad-Najjar aidha amesisitiza kuwa, kura zitaanza kuhesabiwa baada tu ya upigaji kura kumalizika na kwamba katika duru hii ya uchaguzi jitihada zitafanywa ili matokeo yatangazwe haraka iwezekanavyo.

No comments: