Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ametoa wito kwa viongozi wa nchi za
Jumuiya ya Afrika Mashariki kuweka sera madhubuti zitakazoshajiisha
utegemezi wa ndani katika masuala mbalimbali hususan uwekezaji. Rais
Kenyatta amesema wawekezaji wa kigeni wameanza kupungua barani Afrika
kutokana na matatizo ya kiuchumi yanayozikabili nchi zao na kwa mantiki
hiyo pana haja ya kuboresha mazingira kwa ajili ya kuinua uwekezaji wa
ndani.
Kauli ya rais wa Kenya imetolewa huku maoni na hisia mbalimbali
zikiendelea kujitokeza siku moja baada ya nchi za Afrika Mashariki
kusoma kwa pamoja bajeti zao za mwaka 2013/2014. Nukta inayozikutanisha
pamoja bajeti hizo ni suala la kuongezwa kodi kwa bidhaa za anasa kama
vile pombe, sigara, simu za mkononi na magari.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment