Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 26, 2013

Usafirishaji wa makaa ya mawe wasitishwa Msumbiji

Kiogozi mmoja nchini Msumbiji amearifu kusimamishwa shughuli za usafirishaji makaa ya mawe katika eneo la mkoa wa kaskazini magharibi nchini humo. Hatua hiyo imekuja kufuatia kuongezeka wasi wasi wa hali ya usalama inayoweza kuikabili sekta ya usafirishaji wa njia ya treni 'Sena' baada ya chama kikuu cha upinzani Renamo kutoa vitisho kuhusiana na suala hilo. Mkuu wa mkoa wa Tete Rachid Gogo, ameiambia redio ya nchi hiyo kuwa maafisa wa shirika la Rio Tinto wameamua kusimamisha shughuli za usafirishaji wa bidhaa hiyo kwa kuhofia hasara inayoweza kuwapata kutokana na vitisho hivyo.
Ni vyema kuashiria hapa kwamba, Shirika la Rio Tinto hujishughulisha na uvumbuaji na uchimbaji madini katika nchi mbalimbali. Hivi karibuni wafuasi wa chama tawala cha Frelimo nchini Msumbiji walifanya maandamano makubwa ya kitaifa siku ya Jumamosi kwa lengo la kulaani hujuma za hivi karibuni zinazodaiwa kutekelezwa na wafuasi wa chama kikuu hicho cha upinzani.

No comments: