Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 19, 2013

Ethiopia, Misri kusuluhisha mzozo wa Mto Nile

Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Mohamed Kamel Amr amesema kuwa nchi yake imekubaliana kuendeleza mazungumzo zaidi na Ethiopia ili kujadili na kutatua mgogoro wa maji ya Mto Nile kwa njia za kidiplomasia. Kamel Amr amesema mazungumzo hayo yatafanyika katika ngazi za kisiasa na kitaalamu ili kutathmini athari zitakazojitokeza iwapo Ethiopia itaamua kuendelea na ujenzi wa bwala la Renaissance.
Msimamo wa Misri unafuatia mkutano wa hapo jana kati ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia na Misri mjini Addis Ababa. Mgogoro huo umepelekea kuzuka vita vya maneno kati ya Cairo na Addis Ababa ambapo Misri huko nyuma ilitishia kutumia nguvu za kijeshi kusimamisha ujenzi wa bwawa hilo. Cairo inadai maji ya Mto Nile ni uti wa mgongo wa uchumi wake na kwamba juhudi zozote za kuipunguzia maji ya mto huo ni sawa na kukata mshipa wake wa pumzi.

No comments: