Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 28, 2013

Mkutano wa kibiashara kuanza leo Dar es Salaam

Zaidi ya viongozi 10 wa nchi na serikali kutoka nchi mbalimbali za dunia wanakutana mjini Dar es Salaam Tanzania kujadili ushirikiano wa kibiashara. Mkutano huo unaojulikana kama Smart Partnership International Dialogue 2013 utafunguliwa rasmi na Rais Jakaya Kikwete alasiri ya leo na miongoni mwa mambo yatakayojadiliwa ni pamoja na jinsi ya kutumia teknolojia ya kisasa kuinua uchumi wa nchi zinazoshiriki. Miongoni mwa marais wanaohudhuria ni pamoja na Uhuru Kenyatta (Kenya), Yoweri Museveni (Uganda), Mahinda Rajapaksa (Sri Lanka), Ikililou Dhoinine (Comoro), Mfalme Mswati II (Swaziland).

No comments: