Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 28, 2013

Kenyatta:Ufisadi upigwe vita vikali

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amewataka maafisa wakuu serikalini kutumia nyadhifa zao kukabiliana na ufisadi.
Akizungumza wakati wa sherehe za kuapishwa Makatibu Wakuu wa wizara mbalimbali hapo jana, Rais Kenyatta alisema ufisadi umelemaza serikali zilizopita na kwamba hayuko tayari kufuata mkondo huo. Amesema serikali yake inataka kufikisha maendeleo kwa mwananchi wa kawaida na ili kufanikisha lengo hilo, sharti ulaji rushwa upigwe vita kwa nguvu zote.
Kuapishwa makatibu hao kunahitimisha mkwamo wa kisiasa ulikuwa ukiripotiwa nyuma ya pazia kuhusu uteuzi wa maafisa hao. Uhuru amesema sasa serikali iko tayari kuanza kazi ya kutekeleza ahadi alizotoa kwa wananchi wakati wa kampeni.
Huku hayo yakijiri, Baraza la Mawaziri hapo jana liliwataka walimu kusitisha mgomo wao wa kitaifa na kufanya mazungumzo na serikali ili kutatua mivutano iliyoko. Mgomo wa kitaifa wa walimu wa shule za umma umeingia siku yake ya nne leo Ijumaa huko nchini Kenya.

No comments: