Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 14, 2013

Kiongozi Muadhamu awaongoza Wairani kupiga kura

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei leo asubuhi ameongoza mamilioni ya Wairani katika zoezi la upigaji kura ambapo amepiga kura yake na kuwataka wananchi waliotimiza masharti ya kupiga kura wajitokeze kwa wingi kutekeleza haki yao ya kidemokrasia. Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema punde baada ya kupiga kura kwamba, maadui wa Iran wamejaribu kutumia kila njia kuwashawishi wananchi kutoshiriki uchaguzi wa rais lakini njama zao zimefeli na zitazidi kufeli kwani idadi iliyoshuhudiwa hadi sasa katika vituo vya kupigia kura ni kubwa mno.
Ayatullah Khamenei amesema matokeo ya mwisho yatadhihirisha wazi mapenzi ya Wairani kwa nchi yao na imani walionayo kwa mfumo. Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa saa mbili asubuhi na hadi sasa foleni ndefu za wapiga kura zinaendelea kuonekana katika maelfu ya vituo hapa Tehran na nchi nzima kwa ujumla. Duru ya 11 ya uchaguzi wa rais imewavutia wagombeaji 6 ambao ni; mwakilishi mkuu wa Iran katika mazungumzo ya nyuklia Saeed Jalili,   kamanda wa zamani wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu Mohsen Rezai, mwakilishi wa zamani wa Iran katika mazungumzo ya nyuklia Sheikh Hassan Rohani, waziri wa zamani wa Mawasiliano Mohammad Gharazi, meya wa Tehran Mohammad Baqer Qalibaf na waziri wa zamani wa Mambo ya Nje Ali Akbar Velayati.

No comments: