Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Ali Akbar Salehi amelaani jinai ya hivi
karibuni iliyofanywa dhidi ya Waislamu wa Kishia nchini Misri na kuonya
kuhusu njama za kuibua machafuko ya kimadhehebu nchini humo. Katika
mazungumzo ya simu na mwenzake wa Misri Mohamed Kamel Amr, Salehi
alilaani mashambulizi ya kinyama yaliyofanywa na watu wanaokufurisha
Waislamu wenzao dhidi ya Waislamu hao wa Kishia. Watu hao wenye misimamo
mikali ya kasalafi walivamia nyumba ya mwanazuoni maarufu wa Kishia
Sheikh Hassan Shehata na kuwaua shahidi Waislamu wanne wa Kishia, Juni
23.
Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri amelaani kitendo
hicho na kusema kuwa, nchi yake haitaruhusu watu wenye misimamo mikali
kuchochea hitilafu za kimadhehebu nchini humo. Naye Msemaji wa Wizara ya
Mambo ya Nje ya Iran Sayyed Abbas Araqchi amesema, maadui wanapanga
kuyasababishia hasara mapinduzi ya Misri kupitia kuibua hitilafu za
kimadhehebu. Amesema maadui awali walijaribu kuibua hitilafu baina ya
Waislamu na Wakristo nchini Misri na sasa wameelekeza njama zao katika
kuibua machafuko baina ya wafuasi wa madhehebu za Kiislamu. Nao wabunge
wa Iran wametoa taarifa na kulaani mauaji ya Waislamu hao wa Kishia huko
Misri baada ya kushambuliwa na watu wenye misimamo mikali ya Kisalafi.
Wametoa wito kwa wanazuoni katika ulimwengu wa Kiislamu kutonyamazia
kimya jinai hiyo. Wabunge wa Iran wamesema, Marekani ndiyo inayofaidika
wakati inapotokea mizozo baina ya Waislamu duniani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment