Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 19, 2013

Hollande: Iran ishirikishwe mkutano wa Geneva 2

Rais Francois Hollande wa Ufaransa amesema kuwa nchi yake itakuwa ya kwanza kumkaribisha rais mteule wa Iran kwenye makutano wa kimataifa wa Geneva 2 wa kujadili mgogoro wa Syria. Hollande amenukuliwa na vyombo vya habari akisema, Sheikh Hassan Rohani aliyechaguliwa kwenye uchaguzi wa rais uliofanyika Ijumaa iliyopita hapa nchini ni mwanadiplomasia mtajika na kwamba anaweza kuleta mitazamo yenye kukubalika kwennye mkutano huo.
Mgogoro wa Syria umetawala vikao vya wakuu wa nchi tajiri zaidi duniani huku Russia ikisisitiza kwamba mgogoro huo utafutiwe ufumbuzi wa kisiasa. Hata hivyo Marekani ambayo pia ilishiriki mkutano huo wa G8 huko Ireland Kaskazini bado inasisitiza kwamba itawapa misaada ya silaha magaidi wanaopigana kuipindua serikali ya Rais Bashar Asad.

No comments: