Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 29, 2013

Mugabe: Sitaondoka kwa mashinikizo ya Magharibi

Rais Robert Mugabe
Rais Robert Gabriel Mugabe wa Zimbabwe amesema kuwa, anakusudia kung'atuka madarakani lakini bila ya kuzingatia matakwa na mashinikizo yanayotolewa na nchi za Magharibi. Kwenye mahojiano aliyofanyiwa na gazeti la serikali la Herald la nchini humo, Rais Mugabe amesema kuwa, sababu kuu ya kuendelea kubaki madarakani kwa zaidi ya miaka 30 sasa, ni kukabiliana na njama za nchi za Magharibi za kutaka kubadilisha muundo wa uongozi nchini humo.
Rais Mugabe mwenye umri wa miaka 89, ameiongoza Zimbabwe tokea ilipojipatia uhuru kutoka kwa mkoloni Muingereza mwaka 1980. Rais wa Zimbabwe amesema kuwa, hatasalimu amri mbele ya mashinikizo ya nchi za Magharibi ya kumtaka aondoke madarakani. Amesema, ataondoka madarakani pindi atakapoona chama chake cha Zanu PF kina umoja na mshikamano zaidi. Uchaguzi ujao wa rais nchini Zimbabwe unatarajiwa kufanyika Agosti 14, na Mugabe atachuana vikali kwenye uchaguzi huo na hasimu wake wa kisiasa Morgan Tsvangirai kutoka chama cha MDC ambaye pia ni Waziri Mkuu wa serikali ya umoja wa kitaifa nchini humo.

No comments: