Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, January 24, 2013

Wabunge wa Maziwa Makuu Afrika wajadili amani

Mkutano wa tatu wa wabunge wa nchi za Maziwa Makuu unaendelea huko Kinshasa mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Katika kikao hicho, washiriki kutoka nchi 12 za Maziwa Makuu wanajadili njia za kurejesha amani ya kudumu kwenye maeneo yenye migogoro ikiwemo Jamhuri ya Afrika ya Kati, mashariki mwa DRC, na baina ya Sudan na Sudan Kusini.
Kikao hicho kilichoanza Jumanne kinatazamiwa kumalizika leo Alkhamisi. Katibu mtendaji wa mkutano wa kimataifa kwa nchi za Maziwa Makuu, Ntumba Luaba ametoa wito kwa washiriki kuhakikisha kuwa wanajitahidi kupitisha maazimio ambayo yatahakikisha makundi yanayovuruga amani katika eneo la Maziwa Makuu yanatokomezwa ifikapo mwaka 2014. Amesema kushughulikiwa masuala ya usalama ni jambo ambalo litatoa fursa kwa harakati za kutokomeza umaskini.

No comments: