Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, January 24, 2013

Mchunguzi wa mauaji ya Tana Kenya ashambuliwa

Jaji mmoja katika Mahakama Kuu ya Kenya anayechunguza mauaji ya eneo la Tana Delta nchini humo ameshambuliwa na genge la wezi nyumbani kwake.
Duru zinadokeza kuwa Jaji Bi. Grace Nzioka alikuwa akiendesha gari karibu na nyumbani kwake katika mtaa wa Karen saa nne usiku jana Jumatano wakati aliposimamishwa na genge la watu watano waliokuwa na silaha nzito.
Jaji huyo ni mwenyekiti wa  tume inayochunguza mapigano ya eneo la Tana Delta ambapo zaidi ya watu 160 wameuawa katika kipindi cha miezi sita iliyopita na maelfu ya wengine kuachwa bila makao.
Baada ya kumchukua jaji huyo mateka, genge hilo liliingia nyumbani kwake na kupora nyaraka kadhaa, laptop na televisheni. Polisi wanachunguza tukio hilo na wanahoji ni kwa nini walinzi wawili wa jaji huyo hawakuwa wamebeba silaha wakati wa tukio hilo. Mapigano katika eneo la Tana Delta ni baina ya makabila mawili makuu hasimu ya Orma na Pokomo. Baadhi ya duru nchini Kenya zinasema mapigano hayo yamechochewa na uamuzi wa serikali ya Qatar wa kukodi ardhi zenye rotuba katika eneo hilo kwa ajili ya kilimo.

No comments: