Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, January 24, 2013

Al Shabab watishia kuwaua mateka Wakenya

Waasi wa Somalia wa al Shabab wameitaka Kenya kuwaachilia huru Waislamu wote wanaoshikiliwa kwa tuhuma za ugaidi na kutishia kuwa takwa hilo lisipotekelezwa watawaua mateka wote wa Kenya wanaowashikilia.
Waasi hao wametuma kwenye mtandao wa Tweeter video ya Wakenya wawili waliowateka nyara katika kaunti ya Wajir mwaka uliopita na kuiambia serikali ya Kenya kwamba maisha yao yapo hatarini.
Wiki iliyopita waasi wa al Shabab wa Somalia walisema kwamba wamemuua Denis Allex, jasusi wa Ufaransa waliokuwa wanamshikilia mateka, ili kulipiza kisasi kutokana na kile walichoeleza kuwa ni uadui wa Ufaransa kwa Waislamu na mashambulizi yake ya kijeshi nchini Mali.
Kenya inawashikilia watu kadhaa wanaodaiwa kuwa na uhusiano na kundi la as Shabab  na kuhusika katika mashambulizi ya kigaidi nchini humo.

No comments: