Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, January 25, 2013

Mawakili wa Takukuru watinga Kortini nusu uchi

WAKILI wa Kujitegemea Ademba Gomba aliwaumbua waendesha mashtaka wawili wa Tasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa kuiomba Mahakama isiwatambue uwakilishi wao, hadi wakavae vizuri.
Omary The Great ilishuhudia mawakili hao wa kike, Hellen Osujaki  na Faraja Sambala wakitinga Mahakamani wakiwa wamevaa nusu uchi hususan sehemu za vifuani zikionekana hata jinsi cheni zao zilivyokuwa zimekaa ilikuwa ni aibu tumu.
Kabla ya kesi kuanza watu waliokuwa katika Mahakama hiyo ya Hakimu Mkazi Kisutu wakiwemo washtakiwa walishindwa kuvumilia  aibu hiyo kiasi cha kuguna na kusema "Duh aibu gani hii".
Kitendo hicho kilimfanya Wakili  Ademba aiombe  Mahakama isitambue uwepo wa uwakilishi wa mawakili hao wa Takukuru Mahakamani hadi hapo watakaporekebisha mavazi yao kwa kuvihifadhi vifua vyao.

Baada ya kutolewa kwa ombi hilo, Hakimu Victoria Nongwa aliyekuwa amepangiwa kuisikiliza kesi hiyo, aliisimamisha kesi kwa muda wa dakika 10 ili kuwapa nafasi mawakili hao wa Takukuru kuvaa vizuri nguo zao.
Hivyo watu wote pamoja na washtakiwa walitoka nje na ulipomalizika muda huo, mawakili hao walirudi wakiwa wamevaria nadhifu na mahakama ikaendelea.
Katika kesi hiyo,  vigogo watatu wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam walipandishwa kwenye mahakama hiyo, wakikabiliwa na mashtaka ya kula njama, wizi na kuisababishia serikali hasara ya mamilioni ya fedha.
Vigogo hao wanadaiwa kujipatia fedha hizo kutokana na kukusanya mapato katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo ,Washtakiwa hao ni Mhasibu  Msaidizi  na Afisa Maalipo Mkuu wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam.
Wengine ni Elida  Mponda, Mhasibu  na Mkusanya wa Mapato wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam, Geofrey Kibasa na  Afisa wa Mapato wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salam, Ernest Maduhu .

No comments: