Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, January 22, 2013

ILO yatabiri kuongezeka idadi ya wasio na ajira


Ripoti ya Shirika la Kazi Duniani (ILO) inaonesha kuwa, idadi ya watu wasio na ajira inatarajiwa kuongezeka mwaka huu na kufikia milioni 202. Ripoti ya kila mwaka ya Shirika la Kazi Duniani iliyotolewa leo imebainisha kuwa, ikiwa imepita miaka mitano tangu kuibuka mgogoro wa fedha duniani, idadi ya watu wasio na ajira inazidi kuongezeka na kwamba, walimwengu wataraji kuona idadi hiyo ikifikia milioni 202 katika mwaka huu wa 2013.

Aidha ripoti hiyo imezungumzia mwenendo wa ajira duniani na kubainisha kwamba, mwaka jana takribani watu milioni nne waliongezeka katika idadi ya watu wasio na kazi ulimwenguni na kuifanya idadi hiyo kufikia watu milioni 197.  Ripoti ya Shirika la Kazi Duniani inaeleza kuwa, mgogoro wa kiuchumi na matatizo ya fedha yaliyotokea barani Ulaya ndilo chimbuko kuu la kuongezeka kwa kasi idadi ya watu wasio na kazi duniani; kwani kabla ya mgogoro huo idadi ya watu wasio na kazi duniani ilikuwa milioni 28 tu.

No comments: